Yanga inahusishwa kumuwania kiungo mshambuliaji wa Al Hilal Makabi Lilepo ambaye msimu uliomalizika alipachika mabao manne katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Lilepo ni miongoni mwa wachezaji ambao wameomba kuondoka Al Hilal kufuatia machafuko yanayoendelea nchini humo
Wakati huohuo, Yanga inahusishwa na kocha wa Al Hilal Florent Ibenge, Wananchi wanaweza kuwa na nafasi nzuri ya kumpata Lilepo kama Ibenge atatua nchini

Imeelezwa Ibenge tayari amevunja mkataba na Al Hilal wakati Lilepo bado wanamuwekea ngumu wakitaka wamtoe kwa mkopo
Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa Yanga kujaribu kuinasa saini ya winga huyo mwenye kasi
Kabla ya kutua Al Hilal Yanga ilijaribu kumsajili msimu uliopita lakini ofa nono ya Al Hilal ikapelekea Mcongomani huyo kutimkia Sudan ambako hata hivyo sasa hatamani tena kurudi kutokana na vita inayoendelea
Mahusiano mazuri ya Yanga na wachezaji kutoka DR Congo inaweza kuwa chachu kwa mshambuliaji huyo kutua Yanga



