Mbeya - Local

Mbeya City yafuta kiingilio mechi dhidi ya Mashujaa Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Jun 2023
Mbeya City yafuta kiingilio mechi dhidi ya Mashujaa Fc

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Juma Zuber Homera amesema kuwa kuelekea mchezo wa marudiano kati ya Mbeya City dhidi ya Mashujaa hatua ya mtoano(play off) hakutakuwa na kiingilio ili kutoa nafasi kwa mashabiki kuingia kwa wingi uwanjani na kuipa hamasa timu yao

Homera amesema baada ya timu hiyo kuchapwa mabao 3-1 na Mashujaa Fc katika mchezo wa kwanza wa play-off uliopigwa mkoani Kigoma,  wanapaswa kushikamana kipindi hiki ambacho Mbeya City inapatia mazingira magumu ya kupambana ili kusalia ligi kuu Tanzania bara

"Matokeo ya kule Kigoma sio mazuri,inapaswa tushirikiane kwa pamoja ili kuinusuru timu yetu, niwaombe sana mashabiki wa soka na wadau tufike kwa wingi uwanjani, hakutakuwa na kiingilio yaani bureee,tuujaze uwanja wa Sokoine ili tupindue matokeo," alisema Homera

Mchezo wa marudiano Kati ya Mbeya City dhidi ya Mashujaa hatua ya Play off umepangwa kuchezwa June 22, 2023 katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya

Mbeya City wanahitaji kupata ushindi wa goli 2-0 baada ya mchezo wa kwanza kupoteza kwa mabao 3 - 1 Lake Tanganyika Kigoma.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’