Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Juni 23 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd June 2023


Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Juni 23 2023

Mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah, 31, ndiye mchezaji mwingine anayesakwa na Saudi Pro League baada ya kuwasili kwa Karim Benzema na N'Golo Kante. (Four Four Two)

Wakala wa Jurgen Klopp amepuuzilia mbali tetesi kwamba kocha huyo mkuu wa Liverpool anaondoka Anfield kwenda kuchukua mikoba ya Hansi Flick kama kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani. (Mirror)

AC Milan wanatumai kuwashinda mahasimu wao Inter Milan katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Romelu Lukaku, 30, (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Manchester United wameafikiana na Chelsea kuhusu dili la la kumsajili kiungo wa Uingereza Mason Mount, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 akikaribia kununuliwa kwa pauni milioni 60. (Mirror)

Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta anaamini kuwa kiungo wa Uingereza Declan Rice, 24, ndiye nahodha wa baadaye wa klabu hiyo na The Gunners wanajiandaa kuwasilisha ofa ya tatu hivi karibuni na mahitaji mengine ya West Ham. (Mail)

Rice bado ana nia ya kujiunga na Arsenal licha ya Manchester City kuonyesha nia ya kujiunga na kinyang'anyiro hicho na washindi wa Treble pia kuweza kukidhi bei ya £100m. (Guardian)

Tottenham wameibuka kuwa mstari wa mbele kumsajili kiungo wa kati wa Leicester City na Uingereza James Maddison, 26. (Guardian)

Bayern Munich wako tayari kumpa mkataba wa miaka miwili beki wa kulia wa Manchester City na Uingereza Kyle Walker, 33. (Bild - Kwa Kijerumani)

Fulham wanaongoza kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa Southampton na England James Ward-Prowse, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 akiwa tayari kuhamia Craven Cottage baada ya Saints kushushwa daraja kutoka Ligi ya Premia. (Independent)

Borussia Dortmund wanapanga kutoa kitita cha pauni milioni 13 kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United na Tunisia Hannibal Mejbri, 20, ambaye msimu uliopita alichezea Birmingham kwa mkopo . (Manchester Evening News)

Klabu hiyo ya Bundesliga pia inamtaka kiungo wa kati wa Manchester City Cole Palmer, 21, huku Dortmund wakitafuta mbadala wa Jude Bellingham. (Bild - kwa Kijerumani)

Manchester United imeipatia Roma nafasi ya kumsajili kiungo wa kati wa Uholanzi Donny van de Beek, 26. (Metro)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.