Zinavuna kila kona tetesi kuhusu kiungo Jonas Mkude ambaye hataendea kuitumikia klabu ya Simba baada ya mkataba wake kumalizika na timu hiyo kutangaza kuachana nae
Zipo taarifa za ndani kuwa mabosi wa Yanga wanaweza kumpa Mkude mkataba wa mwaka mmoja wakiamini anaweza kuongeza kitu katika kikosi cha Yanga
Mkude ni miongoni mwa viungo bora walioyajenga majina yao katika soka la Tanzania kwa muda mrefu
Yawezekana kwa sasa sio yule Mkude wa misimu kadhaa iliyopita lakini bado ni mchezaji anayeweza kuongezea timu hiyo ubora katika eneo la kiungo
Hata hivyo huku Yanga eneo la kiungo tayari lina Yannick Bangala, Mudathir Yahya, Khalid Aucho, Salum Abubakar na Zawadi Mauya huku Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe akitamba kuna namba 6 mwingine matata atatambulishwa wiki ijayo
Ni wazi kama Yanga itamsajili Mkude atakuwa na kazi ya kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha mabingwa hao wa Tanzania Bara kwa misimu miwili mfululizo
Mkude alipata mafanikio makubwa wakati akiwa Simba, kabla ya msimu uliopita, alikuwa na uhakika wa kupata nafasi ya kucheza karibu kila mechi katika kikosi kilichokuwa kimesheheni wachezaji bora