Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Salim Abdallah 'Try Again' amesema mipango ambayo klabu imeweka katika michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao ni kucheza nusu fainali
Akizungumza katika hafla ya chakula iliyoandaliwa na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mkoani Dodoma jana, Try Again alisema Simba itasajili wachezaji wenye ubora mkubwa ili kuweza kufikia malengo
"Lengo kuu ni kuhakikisha tunacheza hatua ya nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa hivyo tutafanya usajili mkubwa kuelekea msimu ujao ili kuweza kutimiza malengo yetu," alisema Try Again
Aidha Try Again alibainisha kuwa pamoja na kukosa mataji katika misimu miwili iliyopita, Simba imekusanya mataji mengi kuliko timu yoyote hapa Tanzania katika miaka mitano iliyopita
"Hatukufanya vibaya katika miaka mitano iliyopita, katika makombe 16 tuliyoshindania, Simba ilishinda makombe 13," aliongeza Try Again
Katika hatua nyingine, Mtendaji Mkuu wa Simba Imani Kajula alibainisha kuwa katika mipango waliyojiwekea msimu ujao, Bajeti ya klabu itafikia Tsh Bilioni 23



