Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Julai 01 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Julai 01 2023

Luis Enrique atafanya dau kwa ajili ya winga wa Manchester City na Ureno Bernardo Silva, 28, kuwa kipaumbele chake atakapochukua nafasi ya Christophe Galtier kama mkufunzi wa Paris St-Germain . (90min)

Kocha huyo wa zamani wa Uhispania pia anataka PSG kumsajili mshambuliaji wa Ureno Joao Felix, 23, kutoka Atletico Madrid. (Relevo – in Portugal)

Manchester United inamlenga mshambuliaji wa Porto wa Iran Mehdi Taremi, 30. (Jornal de Noticias – in portuguese)

Chelsea wanakaribia kufikia makubaliano na Inter Milan kuhusu uhamisho wa kudumu wa mshambuliaji wao wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 30. (90min)

Chelsea wamekubali kumruhusu mlinzi wa Uhispania Cesar Azpilicueta, 33, kujiunga na Atletico Madrid kwa uhamisho wa bila malipo. (Marca kwa Kihispania)

West Ham wanatumai kukubaliana na Arsenal kuhusu malipo ya pauni milioni 105 kwa kiungo wao wa kati Declan Rice, 24, kufikia Jumatatu. (Sun)

Kocha wa Roma Jose Mourinho anataka kumsajili kiungo wa kati wa Brazil Fred, 30, kutoka klabu yake ya zamani ya Manchester United . (Sun)

Christian Pulisic wa Chelsea amekubaliana kimsingi kuhusu mkataba wa muda mrefu wa kujiunga na AC Milan, lakini klabu bado hazijakubaliana kuhusu ada ya uhamisho wa winga huyo wa Marekani, 24. (ESPN)

Pendekezo la Hakim Ziyech kuhama kutoka Chelsea kwenda Al Nassr limezimwa baada ya winga huyo wa Morocco, 30, kushindwa kufikia vigezo katika vipimo vya afya. (Mail)

Ziyech alipewa ofa mpya huku mshahara wake wa kimsingi ukipunguzwa kwa 40%, lakini amekataa. (CBS)

Chelsea wataongeza juhudi zao za kumsajili kiungo wa Ecuador Moises Caicedo, 21, na wanatumai kuwa ada ya takriban £80m inaweza kuafikiwa na Brighton . (Standard)

Manchester United italazimika kuuza kabla ya kumnunua mlinda mlango wa Inter Milan raia wa Cameroon Andre Onana, 27. (Talksport)

United imemtaka mlinda mlango wa Uhispania David de Gea, 32, ambaye mkataba wake katika Old Trafford umemalizika hivi punde, asijiunge na klabu nyingine iwapo hawataweza kupata mlinda mlango mpya ndani ya bajeti yao ya uhamisho. (Sun)

Fulham wanataka pauni milioni 60 kumnunua kiungo wa kati wa Ureno Joao Palhinha, 27, ambayo itakuwa ada ya rekodi ya klabu kwa West Ham . (Football Insider)

West Ham wako kwenye mazungumzo ya kiwango cha juu na Leicester City kwa ajili ya kumchukua winga wa Uingereza Harvey Barnes, 25. (90min)

Manchester United watasalia na £65mza kumnunua mshambuliaji mpya mara watakapokamilisha usajili wa kiungo wa kati wa Chelsea na Uingereza Mason Mount, 24. (Mail)

Bayer Leverkusen huenda ikalazimika kuboresha ofa yao kwa Arsenal ikiwa wanataka kukamilisha usajili wa kiungo wa kati wa Uswizi Granit Xhaka, 30. (Mirror)

Bayer Leverkusen huenda ikalazimika kuboresha ofa yao kwa Arsenal ikiwa wanataka kukamilisha usajili wa kiungo wa kati wa Uswizi Granit Xhaka, 30. (Mirror)

Mshambuliaji wa Brazil Angelo Gabriel, 18, amekamilisha sehemu ya kwanza ya matibabu yake baada ya kukubali kujiunga na Chelsea kutoka Santos kwa kandarasi ya miaka sita. (Fabrizio Romano)

Chelsea wamempa mkataba mpya beki wao wa kati Levi Colwill mwenye umri wa miaka 20. (Standard)

Wakala wa Marc Cucurella amepuuzilia mbali ripoti ya gazeti la Uhispania la Marca kwamba Chelsea wamempa beki huyo wa kushoto wa Uhispania, 24, kwa Atletico Madrid kama "habari za uwongo". (Metro)

Willian amekataa ofa ya Fulham ya kuongeza mkataba wa mwaka mmoja huku winga huyo wa zamani wa Brazil, 34, akifuatilia kwa karibu ofa zingine za Ligi ya Premia. (Standard)

Beki wa Fulham Muingereza Tosin Adarabioyo, 25, anasalia kuwa juu kwenye orodha ya Tottenham ya wachezaji wanaoweza kusajiliwa na beki wa kati msimu huu. (Football London)

Manchester City itamruhusu Zack Steffen kuondoka msimu huu wa kiangazi huku Leicester City wakionyesha nia ya kumnunua mlindalango huyo wa Marekani, 28. (ESPN)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.