Kiungo Dominik Szoboszlai raia wa Hungary aliyejiunga na Liverpool amekabidhiwa jezi nzito namba 8 iliyokuwa ikivaliwa na nahodha Steven Gerrard
Szoboszlai ametua Liverpool kwa mkataba wa miaka mitano dau lake likiwa €70m
Baada ya uhamisho wake kukamilika, nyota huyo ameweka wazi kwa nini amependa kutumia jezi namba nane
“Nina tatoo ya Steven Gerrard hiyo ndio sababu ya kwanini alikuwa mkubwa kipindi niko mdogo"
"Klopp? ndio aliniita ni kweli. Nikasema ni sawa, hili jambo litaenda kuwa bora sana na kila kitu kilikuwa sawa." alisema Szoboszlai.



