Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Julai 04 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Jul 2023
Tetesi za soka Ulaya, Julai 04 2023

Bayern Munich wanapanga kuwasilisha ofa ya pili kwa klabu ya Tottenham kwa lengo la kumnunua mshambuliaji wao wa Uingereza Harry Kane, 29. (Sky Sport - kwa Kijerumani)

Manchester City wanatayarisha ofa yao ya kwanza kumnunua mlinzi wa Croatia Josko Gvardiol, 21, baada ya kuanza mazungumzo na RB Leipzig. (ESPN)

Kiungo wa Liverpool na Uingereza Jordan Henderson, 33, na mshambuliaji wa Chelsea na Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 34, ni wachezaji wawili wanaoweza kusajiliwa na Al-Ettifaq baada ya klabu hiyo ya Saudia kumteua Steven Gerrard kama mkufunzi wao mpya. (Mail)

Paris St-Germain wanapaniaa kuzishinda Chelsea, Liverpool na Manchester City katika mbio za usajili kiungo wa Uhispania Gabri Veiga, 21, kutoka Celta Vigo. (Guardian)

Chelsea wamefanya mazungumzo na Southampton kuhusu uwezekano wa kumnunua beki wao wa zamani Tino Livramento, 20. Southampton wanamthamini mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza chini ya miaka 21, ambaye pia anawindwa na Newcastle, kwa pauni milioni 38. (Mail)

Liverpool wamepiga hatua mbele ya Chelsea katika kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa kati wa Ubelgiji Romeo Lavia na wanaandaa ofa ya ufunguzi kwa kinda huyo mwenye umri wa miaka 19, ambaye Southampton wanasema ni ya thamani ya £50m. (talkSPORT)

Al-Nassr wametoa ofa nono kwa kipa wa Cameroon na Inter Milan Andre Onana, 27, ambaye pia analengwa na Manchester United. (CBS)

Kiungo wa Arsenal na Uswizi Granit Xhaka, 30, atakamilisha uhamisho wa pauni milioni 21.5 kwenda Bayer Leverkusen wiki hii. (Sun)

Everton wameiambia Almeria kwamba wana nia ya kufikia kipengele cha kuachiliwa kwa El Bilal Toure cha euro milioni 40, ingawa Fulham wanaweza kumnunua mshambulizi huyo wa Mali, 21, ikiwa watamuuza mshambuliaji wa Serbia Aleksandar Mitrovic, 28, msimu huu wa joto. (Sacha Tavolieri)

Christian Pulisic wa Chelsea hana nia ya kuhamia Lyon msimu huu wa joto kwani winga huyo wa Marekani, 24, anapendelea kujiunga na AC Milan baada ya kuafikiana kimsingi na klabu hiyo ya Serie A. (ESPN)

Newcastle wanatafakari uwezekano wa kumnunua beki wa Sporting Lisbon na Ureno Goncalo Inacio, 21. (Football Insider) Brighton wana nia ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Ghana Mohammed Kudus, 22, kutoka Ajax. (Athletic, usajili unahitajika)

Wolves wako tayari kumuuza beki Mwingereza Max Kilman mwenye umri wa miaka 26 msimu huu wa joto, licha ya kukataa ofa kutoka kwa Napoli. (90 min)

Chelsea wanataka kumuuza Callum Hudson-Odoi msimu huu wa joto, huku Nottingham Forest ikiwa miongoni mwa wachezaji wanaopewa nafasi kubwa ya kumsajili winga huyo wa Uingereza, 22. (Football Transfers)

Manchester City wako tayari kulipa Atletico Madrid euro 15m (£12.9m) kwa ajili ya winga wa Uhispania Rodrigo Riquelme, 23, ambaye msimu uliopita alicheza kwa mkopo katika klabu dada ya City Girona. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Leicester City wanatafuta kumnunua beki wa Manchester City Muingereza Callum Doyle, 19. (Athletic, usajili unahitajika)

Bordeaux wanatarajia Josh Maja kuondoka katika klabu hiyo kwani mshambuliaji huyo mzaliwa wa Uingereza, 24, sasa ni mchezaji huru na hajajibu ofa ya kuongezewa mwaka mmoja. (L'Equipe - kwa Kifaransa)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
32m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
44m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’