Kramo atua Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th July 2023


Kramo atua Simba

Winga hatari wa Asec Mimosas Kramo Aubin amesajiliwa Simba kwa mkataba wa miaka miwili

Baada ya kuinasa saini ya Essomba Onana ambaye anamudu kucheza nafasi zote za winga, ujio wa Kramo unakwenda kuimarisha zaidi safu ya ushambuliaji ya Simba

Kibu Denis na Pape Ousmane Sakho watakuwa amepata washindani sahihi katika nafasi zao

Winga huyo anatumia miguu yote kwa ufasaha hivyo kumfanya kuwa mchezaji ambaye Simba inaweza kumtumia katika nafasi zote za winga na hata kiungo mshambuliaji

Ukizungumzia wachezaji waliong'ara katika kikosi cha Asec kilichocheza nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu uliopita, Kramo ni miongoni mwao akipachika mabao manne

Simba haikuanza kumfuatilia Kramo msimu huu, hata msimu uliopita alikuwa kwenye orodha ya nyota waliokuwa wakiwaniwa lakini mpango wa kumnasa haukufanikiwa 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.