Meneja wa Yanga Walter Harrison amesema idadi kubwa ya wachezaji wamerejea nchini kwa ajili ya kuanza maandalizi ya msimu (2023/24)
Walter amesema jana klabu hiyo iliendesha zoezila kupima afya za wachezaji ambalo wanatarajia kulikamilisha hapo leo
Siku ya Jumatano Yanga itaanza rasmi mazoezi Avic Town ambapo kutakuwa na program mbili kwa siku
"Idadi kubwa ya wachezaji wamerejea na leo tumeanza zoezi la kupima afya za wachezaji. Tunatarajia zoezi hilo litakamilika hapo kesho (Jumanne) na Jumatano tutaanza rasmi maandalizi"
"Tunatarajia kuwa na session mbili za mazoezi asubuhi na jioni kuhakikisha wachezaji wanakuwa tayari kwa wakati," alisema Harrison
Akizungumzia uamuzi wa kuweka kambi Avic Town, Harrison amesema yalikuwa mapendekezo yaliyozingatia sababu mbalimbali
"Unajuwa baada ya kumaliza msimu kuna wachezaji walisafiri kwenda mapumziko, kwa kuzingatia muda uliobaki na mapendekezo ya kocha, tukaona haitakuwa nyema kusafiri tena nje ya nchi"
"Hapa Avic Town tuna kila kitu tunachokihitaji kwa ajili ya maandalizi, naamini tutakuwa na maandalizi mazuri hapa"