Simba - Local

CRDB kusajili mashabiki Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Jul 2023
CRDB kusajili mashabiki Simba

Klabu ya Simba leo imeingia makubaliano ya Ushirikiano na Bank ya CRDB katika kusajili Mashabiki wa klabu ya Simba

Akizungumza katika hafla iliyofanyika viwanja vya Leaders leo, Mtendaji Mkuu wa Simba Iman Kajula, amesema Simba inatarajiwa kutoa kadi za aina tatu ambazo zote zitapatikana katika Matawi yote ya CRDB nchi nzima

"Katika ushirikiano wetu na CRDB tutakua kadi za aina tatu, kadi za watoto chini ya umri wa miaka 18,  kadi za mashabiki wa kawaida na kadi za Platinum. Kadi zote zitakua ni Visa ambayo mtu anaweza kufanya miamala popote duniani," alisema Kajula

Aidha kampuni yua CRDB imeanzisha akaunti maalum kwa ajili ya mashabiki wa Simba, akaunti ambayo kwa atakayekuwa nayo atapata bima yenye thamani ya Tsh Milioni 2

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Abdul Majid Nsekela amesema pia wameanzisha akaunti kwa ajili ya kina Mama itakayoitwa Simba Queens Account

"Tumeanzisha Simba Account, Maalumu kwa ajili ya mashabiki wetu, pia tumeanzisha Account kwa ajili ya kina Mama itakayoitwa Simba Queens Account (Account ya Malkia wa Simba) Shabiki wa Simba akiwa na Account hizi atapata Bima yenye thamani ya Shilingi milioni 2," alisema

Viongozi na wadau mbalimbali wa klabu ya Simba walihudhuria hafla hiyo ambayo imefungua ukurasa wa ushirikiano katika ya klabu ya Simba na CRDB

Simba inaarajiwa kufanya tukio la aina hiyo na benki ya NMB

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’