Ni rasmi klabu ya Yanga imemtambulisha kiungo Jonas Mkude kuwa mchezaji wao mpya
Mkude anatua Yanga akiwa mchezaji huru akitokea klabu ya Simba
Ni usajili uoliokuwa umegubikwa na tetesi nyingi lakini hatimaye, Yanga imethibitisha kumnasa kiungo huyo mwandamizi
Yanga imemsajili Mkude baada ya Kocha Mkuu wa timu hiyo Miguel Gamondi kujiridhisha kuwa ni mchezaji anayeweza kuwa na mchango katika kikosi chake