Benki ya CRDB imeingia makubaliano na klabu ya Yanga kudhamini Wiki ya Mwananchi ambayo imeanza rasmi leo na kilele chake kikiwa Julai 22 pale uwanja wa Benjamin Mkapa
Mtendaji Mkuu wa Yanga Andre Mtine amesema wanafurahi kushirikiana na CRDB katika tukio hili kubwa linaloambatana na matukio ya kijamii na burudani
"Tunayo furaha kushirikiana na CRDB katika tukio kubwa la Wiki ya Mwananchi ambalo tutalihitimisha uwanja wa Benjamin Mkapa Julai 22 kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Kaizer Chiefs"
"Mashabiki wetu watapata burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali pamoja na mchezo huu utakaozikutanisha timu zenye historia kubwa barani Afrika"

Naye Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema mashabiki wa Yanga wajiandae kwa Wiki ya Mwananchi ya kihistoria kwani wameandaa burudani ya aina yake
Kamwe amesema mashabiki watapata nafasi ya kuwashuhudia wachezaji wapya katika mechi kubwa dhidi ya Kaizer Chiefs akiamini mchezo huo utaonyesha ubora wa wachezaji hao
"Tumeileta Kaizer Chiefs ambayo ina wachezaji bora kama tulivyo sisi, tunaamini mchezo huu utakuwa kipimo sahihi kwa wachezaji wetu tuliowasajili"
"Sisi hatuleti timu dhaifu ili kuwaaminisha mashabiki kuwa timu yetu ni bora na kusababisha vilio pale ligi inapoanza," alisema Kamwe
Kamwe amesema wanaendelea kutambulisha wachezaji siku ya leo na kesho ambapo utambulisho huo utahitimishwa mwanzoni mwa wiki ijayo kwa kumtambulisha mchezaji jezi namba sita
Wiki ya Mwananchi HII IMEENDAA itazinduliwa rasmi Jijini Mwanza Jumamosi ya tarehe 15 Julai 2023 na kutakuwa na matukio mbalimbali ya kijamii na burudani ya kutosha kwa wananchi Mwanza katika viwanja vya Furahisha