Sio tetesi tena, sasa ni rasmi Yanga imekamilisha usajili wa mlinzi mahiri wa kulia Yao Kouassi Attohoula
Mabingwa wa nchi wamemn'goa Yao Kouassi kutoka klabu ya Asec Mimosas ya Ivovy Coast
Kouassi ni mchezaji kiraka ambaye anaweza kutumika katika nafasi zote za ulinzi na hata kiungo mkabaji
Kwa hakika Yanga imedhamiria kutetea makombe yote, usajili huu unatoa picha halisi ya mipango ya Yanga kuelekea msimu ujao
Kouassi alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Asec kilichotwaa ubingwa wa Ivory Coastl msimu uliopita pamoja na kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC)