Matajiri wa Chamazi, Azam Fc wako Tunisia kwa takribani wiki moja sasa wakiendelea na pre-season kujiandaa na msimu mpya wa mashindano (2023-24)
Azam Fc jana ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Al Hilal ya Sudan ambayo pia iko Tunisia kujiandaa na michuano ya ligi ya mabingwa. Sudan kuna vita hivyo hakuna mashindano ya ligi ya ndani yanayofanyika
Mtanange huo uliopigwa uwanja wa Redes ulimalizika kwa Azam Fc kuibuka na ushindi wa mabao 3-0
Mabao ya Azam Fc yalifungwa na yota wapya Sidibe, Alassane huku bao la tatu likifungwa na Prince Dube




