Nahodha wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo amefuta uwezekano wa kurejea tena kusakata soka barani Ulaya
Aidha Ronaldo ameponda uamuzi wa mishindani wake Lionel Messi kutimkia Marekani akiitaja Ligi ya Marekani kuwa ni dhaifu kuliko ligi ya Saudi Arabia
Kwa mujibu mtandao wa ESPN kauli hiyo aliitoa mara baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Celta Vigo ambapo timu yake ilibugizwa bao 5-0
"Nina uhakika wa 100% siwezi kurudi kwenye klabu yoyote barani Ulaya nina miaka 38 kwa sasa, Mpira wa Ulaya umepoteza ladha yake ligi ambayo inafanya vizuri na ina ubora kwa sasa ni ligi kuu ya England pekee," alisema Ronaldi
Kinara huyo anayeshikilia rekodi ya kupachika mabao mengi katika mashindano yote amesema Ligi ya Saudi Arabia ni bora kuliko ligi ya Marekani na ndio sababu wachezaji wengi wakubwa wanatimkia huko Saudi Arabia na anamini ndani ya mwaka mmoja ligi hiyo itapasua anga zaidi na kuzipita baadhi ya ligi za Ulaya.
Ronaldo alijiuunga na Al Nassr in Desemba 2022 baada ya kuachana na Manchester United na baada ya uhamisho wake nyota wengi wanatua kwenye ligi hiyo