Wachezaji Djuma Shabani na Yannick Bangala ni kama walitikisa kibiriki na wakakuta kimejaa baada Yanga kuwafanyia 'surprise' ya aina yake
Mwezi uliopita baada ya msimu kumalizika nyota hao waliwasilisha barua kwa uongozi wa Yanga wakiomba kuachwa kwenda kusaka changamoto sehemu nyingine
Katika moja ya mahojiano yake, Bangala akabainisha kuwa ana asilimia 20 za kuendelea kuitumikia Yanga
Kwa aina ya usajili ambao Yanga wameufanya ni wazi wachezaji hao hawatakuwa na nafasi katika kikosi cha Kocha Miguel Gamondi msimu ujao
Yao Kouassi kutoka Asec Mimosas amechukua nafasi ya Djuma ambaye anatarajiwa kuibukia TP Mazembe wakati Jonas Mkude huenda akamuondoa Bangala ambaye pia katika nafasi ya beki Yanga imemsajili beki wa Kimataifa wa Uganda, Gift Fred
Bangala alikuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC msimu wa 2021-22, lakini msimu uliopita hakuwa katika ubora na kujikuta akipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza
Hali ilikuwa hivyo kwa Djuma ambaye aliyekuwa kocha wa Yanga Nasreddine Nabi aliamua kuwatumia Kibwana Shomari na Dickson Job katika nafasi yake
Katika ripoti yake ya mwisho, Nabi aliwashauri viongozi wa Yanga kusajili wachezaji mbadala wa Djuma na Bangala