Baada ya winga Luis Miquissone kuvunja mkataba wake na Al Ahly, klabu ya Simba inatarajiwa kumtambulishwa wakati wowote
Miquissone anatua Simba akiwa mchezaji huru baada ya kufikia makubaliano ya kusitisha mkataba wake wa mwaka mmoja uliokuwa umebaki na miamba hao wa soka barani Afrika
Rais wa heshima wa klabu ya Simba Mohammed Dewji 'Mo' amebainisha kuwa klabu hiyo iko mbioni kukamilisha usajili wa Miquissone
Tunakamilisha mambo. pic.twitter.com/KNVuI4WIKQ
β Mohammed Dewji MO (@moodewji) July 20, 2023



