Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Julai 21 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Julai 21 2023

Mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 29, hatasaini mkataba mpya Tottenham. Je, yuko tayari kujiunga na wababe wa Ujerumani Bayern Munich? (Times- usajili unahitajika)

Kane huenda akaondoka Tottenham klabu hiyo ikikubali ada ya uhamisho, lakini hatalazimisha kuhama msimu huu wa joto. (ESPN)

Winga wa Uholanzi Arnaut Danjuma, 26, anatazamiwa kujiunga na Everton kwa mkopo kutoka Villarreal. (Sky Sports)

Aston Villa wamefikia mkataba na Bayer Leverkusen kwa ajili ya winga wa Ufaransa Moussa Diaby, 24. (Birmingham Live)

Tottenham wamewatambua kiungo wa Aston Villa wa Brazil Douglas Luiz, 25, na kiungo wa Chelsea Muingereza Conor Gallagher, 23, kama wachezaji ambao huenda wakachukua nafasi ya Pierre-Emile Hojbjerg wa Denmark, 27, ambaye yuko kwenye mazungumzo ya kujiunga na Atletico Madrid. (Mail

West Ham wanakaribia kushinda mbio za kumnunua Carlos Borges wa Manchester City, ambaye pia anasakwa na Borussia Dortmund na Eintracht Frankfurt, baada ya kutoa pauni milioni 14 kwa winga huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 19. (Guardian)

Manchester City wanamfikiria mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Bradley Barcola, 20, kama mbadala wa Riyad Mahrez. (90 Min) Paris St-Germain pia wanamfuatilia kwa karibu Barcola. (Le Parisien - kwa Kifaransa)

Manchester United wako tayari kuwasilisha ombi lao la ufunguzi kwa Atalanta kumnunua mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund, 20, ambaye pia anasakwa na PSG. (Fabrizio Romano)

Mshambulizi wa Bayern Munich na Senegal Sadio Mane, 31, amekubali mkataba wa kujiunga na klabu ya Al-Nassr ya Saudia Pro League. (90 Min)

Mkufunzi wa Fulham Mreno Marco Silva, 46, amepewa mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya £40m kuinoa klabu ya Saudi Arabia Al-Ahli. (Sky Sports)

Al-Ahli pia wanamlenga kiungo wa kati wa Arsenal wa Ghana Thomas Partey, 30. (Mail)

Brighton wanakaribia kufikia makubaliano ya pauni milioni 15 na Fiorentina kumnunua beki wa Brazil Igor Julio, 25. (Telegraph - usajili unahitajika)

West Ham wameongeza juhudi za kumnunua kiungo wa Southampton Muingereza James Ward-Prowse, 28, na wako tayari kumruhusu kiungo wa kati wa Uingereza Flynn Downes, 24, aende upande mwingine. (Guardian) Kiungo wa kati wa Paris St-Germain na Italia Marco Verratti, 30, analengwa na Liverpool. (Guardian)

PSG wakiamua kumuuza mshambuliaji nyota wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, msimu huu wa joto basi watamtafuta winga wa Manchester City na Ureno Bernardo Silva, 28. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Mkufunzi Erik ten Hag amemwambia mlinzi wa Uingereza Harry Maguire, 30, kwamba hataki aondoke Manchester United, licha ya kumvua unahodha wa klabu hiyo. (Teamtalk)

Crystal Palace, West Ham na Leeds wamesajili nia ya kumsajili Divock Origi kutoka AC Milan lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Saudi Arabia, huku Al-Ettifaq ya Steven Gerrard ikitarajiwa kumpa mshambuliaji huyo wa Ubelgiji, 28, dili "kubwa". (Football Insider)

Mshambulizi wa Albania Armando Broja, 21, anatazamiwa kusalia Chelsea na kupigania nafasi yake msimu ujao, licha ya kuripotiwa kumtaka West Ham. (Express)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.