Klabu ya Kaizer Chiefs ambayo imealikwa na Yanga kushiriki Tamasha la Wiki ya Mwananchi, imewasili nchini
Timu hiyo ilitua uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere na kulakiwa na wenyeji wao Yanga
Yanga na Kaizer Chiefs zitachuana katika mchezo wa kuhitimisha wiki ya Mwananchi kesho Jumamosi saa 1 usiku
Mtanange huo utapigwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Ranga Chivaviro ni miongoni mwa wachezaji waliotua nchini na kikosi cha Kaizer Chiefs
Chivaviro amerudi tena kuikabili Yanga katika uwanja wa Benjamin Mkapa, msimu uliopita akiwa na Marumo Gallants alicheza mechi ya kwanza ya nusu fainali ambayo Yanga ilishinda mabao 2-0