Kocha Mkuu wa Azam Fc Youssouph Dabo amesema kuwa anawapa mbinu mpya wachezaji wake zitakazowafanya wawe wakomavu wa fikira
Timu hiyo ipo kambini nchini Tunisia kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa 2023/24. Jana walicheza mechi ya kirafiki dhidi ya US Monastir na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1
Dabo ambaye ni raia wa Senegel amesema ameona sehemu ambayo wachezaji wake bado hawajawa imara sana ni eneo hilo jambo ambalo wanalifanyia kazi
"Wachezaji wanajituma na ninafurahi wanafuata maelekezo ambacho kipo kwa sasa ni kwenye kuwaongezea mazoezi ya ukomavu wa fikra jambo ambalo kwao lilikuwa chini sana kwenye eneo hilo"
"Ambacho kinafanyika kwa sasa ni kuendelea kuangalia maeneo mengine zaidi ikiwa ni pamoja na kuwapa mazoezi magumu ili wazidi kuwa imara, " alisema
Azam Fc itacheza na Yanga August 09 mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa



