Simba imekamilisha usajili wa mlinda lango Jefferson Luis Szerban de Oliveira raia wa Brazil
Jefferson anajiunga na Simba akitokea klabu ya Resende iliyopo Serie D nchini Brazili
Eneo la mlinda lango ndio nafasi pekee iliyokuwa ikiwaumiza kichwa mashabiki wa Simba
Leo watakuwa na furaha baada ya klabu yao kuthibitisha kumsajili kipa huyo mrefu
Mlinda lango namba moja wa Simba Aishi Manula bado ni majeruhi akitarajiwa kurejea katika majukumu yake mwezi Oktoba 2023