Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limetangaza kufanyika kwa droo ya hatua ya awali kwa Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika, Julai 25, jijini Cairo, Misri kuanzia saa 9:00, saa za Afrika Mashariki
Klabu 54 kutoka mataifa 42 wanachama wa CAF zitashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika, huku klabu 52 kutoka mataifa 41 zikishiriki Kombe la Shirikisho msimu ujao
Droo kwa upande wa Ligi ya Mabingwa itahusisha timu 54, huku mbili kutoka Tanzania Bara zitashiriki mashindano hayo ambazo ni Simba na Yanga na moja kutoka Zanzibar ambayo ni KMKM
Kombe la Shikisho linashirikisha timu 52 huku Tanzania Bara itawakilishwa na Azam FC na Singida fountain Gate FC na kwa Zanzibar itawakilishwa na JKU SC