Simba yamuuza Sakho Ufaransa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th July 2023


Simba yamuuza Sakho Ufaransa

Klabu ya Simba imethibitisha kumuuza winga Pape Ousmane Sakho klabu ya Quevilly Rouen Metropole ya nchini Ufaransa

Sakho hakuwa sehemu ya kikosi kilichosafiri na Simba kwenye pre-season Uturuki akisubiri kukamilika kwa uhamisho wake

Juzi Simba ilitangaza kumrejesha winga Luis Miquissone na jana kutangaza kusajili mlinda lango Jefferson kutoka Brazil

Usajili wa wachezaji hao ulipelekea timu hiyo kuwa na nyota 14 wa kigeni na hivyo kulazimika kuachana na wachezaji wawili

Mchezaji mwingine anayetarajiwa kuachwa na Simba ni Peter Banda ambaye huenda akatolewa kwa mkopo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.