Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Julai 25 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Julai 25 2023

Manchester United iko tayari kuwasilisha ofa rasmi kwa Atalanta kwa ajili ya kumnunua mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund, 20 wiki hii. (Mail)

United wako tayari kulipa £60milioni tu kwa ajili ya mchezaji huyo, ambayo ni pungufu ya euro milioni 100 (£86.5m) wanayoitaka klabu hiyo ya Italia. (Times)

Mashetani wekundu hao pi awanamfuatilia mshambuliaji wa Eintracht Frankfurt mwenye umri wa miaka 24 Mfaransa Randal Kolo Muani, na kocha Erik ten Hag anavutiwa na mshambuliaji mwingine wa Ajax, Mghana Mohammed Kudus, 22, ambaye pia amekuwa akihusishwa na Chelsea. (Mirror)

Ten Hag pia anatarajia kuimarisha safu yake ya ulinzi kwa kusajili golikipa wa akiba wa timu yake. Anamataka mchezaji wa kimataifa wa Uturuki wa Fenerbahce, Altay Bayindir, 25. (Goal)

Chelsea, Manchester United na Tottenham zitakuwa sehemu ya shamrashamra za kutaka kumnunua mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, baada ya Paris St-Germain kupokea ofa ya rekodi ya dunia ya pauni milioni 259 kutoka kwa Al-Hilal ya Saudi Arabia ili kumnunua mchezaji huyo. (Telegraph)

Al Hilal wanapanga kumpa Mbappe mshahara wa jumla wa euro 200m (£172m) kwa mwaka huku wakimruhusu kuwa na asilimia 100% ya haki zake zote za picha kwenye matangazo (Fabrizio Romano)

Iwapo Mbappe atajiunga na Al-Hilal inaweza kuwa mwaka mmoja pekee, huku PSG ikiwa na imani kwamba rais wa Real Madrid Florentino Perez na mchezaji huyo tayari wana makubaliano ya kuhamia La Liga mwaka ujao. (Times)

Barcelona wamekaa kando kwenye sakata la kumnunua Mbappe licha ya madai kuwa walifanya mazungumzo na PSG. (Marca)

Ikiwa Mbappe atahamia Saudi Arabia basi PSG itafikia thamani ya pesa inayotaka Tottenham ya pauni milioni 100 kwa ajili ya mshambuliaji Harry Kane, 29, ingawa Bayern Munich bado wana imani nahodha huyo wa England atachagua kwenda Ujerumani. (Independent)

Klabu ya Saudi Arabia Al Hilal inakaribia kufikia makubaliano na Fulham ya kumsajili mshambuliaji wa Serbia Aleksandar Mitrovic mwenye umri wa miaka 28 (90min)

Kiungo wa kati wa England Jordan Henderson, 33, amewaaga wafanyakazi na wachezaji wenzake katika klabu ya Liverpool kabla ya uhamisho wake wa kujiunga na klabu ya Saudia ya Al-Ettifaq kukamilishwa. (Mail)

Everton wanakaribia kumnasa mshambuliaji wa Almeria El Bilal Toure, 21, licha ya ushindani kutoka kwa klabu ya Atalanta inayomtaka pia mchezaji huyo wa kimataifa wa Mali. (Football Insider)

Tottenham na West Ham zinaongoza katika kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa kati wa England Conor Gallagher, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 akiwa tayari kuondoka Chelsea. (Standard)

Jaribio la Chelsea kumsajili kiungo wa kati wa Ecuador Moises Caicedo, 21, kutoka Brighton limekwama kutokana na ombi la Seagulls kutaka beki mwenye umri wa miaka 20 Levi Colwill kujumuishwa katika mpango huo. (Guardian)

Spurs na Nottingham Forest zote zimefuata Juventus kutaka kumsajili beki wa pembeni wa Italia Andrea Cambiaso, 23. (Tuttosport)

Inter Milan wamepeleka Aston Villa ofa ya Euro 15m (£12.95m) kwa ajili ya mlinda mlango wa Argentina Emiliano Martinez, 30, kufuatia Andre Onana kuhamia Manchester United. (TyC Sports Argentina)

Kiungo wa kati wa Leicester City Hamza Choudhury, 25, anataka mustakabali wake wa muda mrefu utatuliwe mwanzoni mwa msimu huu huku kukiwa na ofa inayotaka kuwasilishwa na Southampton. (Mail)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.