Kikosi cha Azam Fc kinaendelea kujifua katika mji wa Sousse nchini Tunisia yakiwa maandalizi ya msimu mpya. Kocha mkuu wa timu hiyo, Msenegal Youssouph Dabo amewamwagia sifa mastaa wake kwa kuonyesha kiwango cha juu
Azam Fc leo inatarajiwa kucheza mechi ya nne ya kirafiki dhidi ya Stade Tunisien ikiwa imeshinda mechi mbili dhidi ya Al Hilal (3-0) na US Monastir (2-1) na kupoteza mchezo dhidi ya Esperance (0-3)
Dabo ameeleza kufurahishwa na kiwango kinachoonyeshwa na wachezaji wake huku akitamba kuwa timu hiyo imeimarika
"Nafurahi kuona wachezaji wakijituma bila kuchoka na kuhakikisha wanafanya yale tunayowaelekeza, nawapongeza kwa hilo. Tumekuwa na vipindi tofauti tukifanya mazoezi ya nguvu na mbinu kwa nyakati tofauti"
"Katika mechi za kirafiki tunachokiangalia zaidi siyo matokeo bali ni namna gani wachezaji wetu wamepokea na kufanyia kazi kile tulichowaelekeza mazoezini. Kwa kiasi fulani wamefanya vizuri lakini tunaendelea kuwajenga ili kufanya vizuri zaidi. Kila hatua tunayopiga kuna kitu kinaongezeka na mwisho tutakuwa na timu imara msimu ujao," alisema Dabo



