Dirisha la usajili CAF kufungwa Jumatatu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th July 2023


Dirisha la usajili CAF kufungwa Jumatatu

Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limezikumbusha klabu za Yanga, Simba, Azam Fc na Singida FG kukamilisha michakato yao ya usajili kwani dirisha la CAF linakaribia kufungwa

Dirisha hilo linatarajiwa kufungwa siku ya Jumatatu, Julai 31. Klabu zinazoshiriki Ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho zinapaswa kukamilisha usajili wake ndani ya muda huo

Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF, mpaka sasa Singida FG na Simba zimesajili wachezaji 29, Azam Fc imesajili wachezaji 25 huku Yanga ikiwa imesajili wachezaji 24

Yanga na Simba zitashiriki ligi ya mabingwa wakati Azam Fc na Singida FG zitashiriki kombe la Shirikisho

Kila timu inaruhusiwa kusajili hadi wachezaji 40 kwa ajili ya mashindano ya CAF


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.