klabu ya Fc Barcelona imeruhusiwa kwa muda kucheza Ligi ya Mabingwa 2023-24 huku kukiwa na uchunguzi wa Uefa kuhusu madai kuwa klabu hiyo ilitoa hongo kwa mkuu wa waamuzi
Mnamo Machi, bodi inayosimamia soka ya Ulaya ilithibitisha kuwa inachunguza madai ya malipo yaliyotolewa na Barcelona ili kupata maamuzi mazuri ya waamuzi
Barcelona wamekana kufanya makosa hayo. Wakati ikitoa ruhusa hiyo kwa muda, Uefa ilihifadhi haki ya kuiadhibu klabu hiyo siku zijazo
Uchunguzi wa Uefa ulikuja baada ya uchunguzi wa uhalifu kuletwa na ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma wa Barcelona tarehe 10 Machi
Ilidaiwa kuwa Barcelona ililipa euro 8.4m (£7.4m) kwa Jose Maria Enriquez Negreira, makamu wa rais wa zamani wa kamati ya waamuzi wa Uhispania na kampuni yake ya Dasnil 95