AS Vita yatua Singida kuikabili Singida FG

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st July 2023


AS Vita yatua Singida kuikabili Singida FG

Kikosi cha AS Vita kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, kimewasili mkoani Singida kwa ajili ya mchezo wa Singida Dy dhidi ya Singida Fountain Gate

Mchezo huo utapigwa siku ya Jumatano, August 02 katika uwanja wa LITI

Singida FG itatumia mchezo huo kutambulisha kikosi chake kwa ajili ya msimu wa mashindano 2023/24

AS Vita wameweka kambi ya siku 14 Tanzania kujiandaa na msimu mpya

Juzi walicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namungo Fc mkoani Arusha na kukubali kipigo cha bao 1-0


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.