Arsenal wamefikia mkataba kimsingi na Brentford kwa ajili ya mlinda lango David Raya, 27, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania akikadiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 40. (Evening Standard)
Manchester City wanamtaka winga wa Rennes kutoka Ubelgiji Jeremy Doku, huku klabu hiyo ikimtazama mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 kama mbadala wa Riyad Mahrez, ambaye alijiunga na Al-Ahli ya Saudi wiki iliyopita. (Fabrizio Romano)
Manchester City pia inamwona mshambuliaji wa Crystal Palace Michael Olise, 21, kama chaguo kuchukua nafasi ya Mahrez, huku mkufunzi wa Palace Roy Hodgson akikiri kuwa itakuwa vigumu kumbakisha mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa chini ya miaka 21 katika klabu hiyo msimu huu. (Athletic - Usajili unahitajika)
Dau la Bayern Munich la pauni milioni 85 kumnunua mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane limekataliwa, huku Spurs wakitaka zaidi ya pauni milioni 100 kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30. (Independent)
Kane anatarajia kusalia Tottenham msimu huu ikiwa klabu hiyo haitaafikiana na Bayern kabla ya mechi ya kwanza ya Ligi Kuu dhidi ya Brentford, kwani anaamini itakuwa si haki kuondoka baada ya kuanza kwa kampeni. (Evening Standard)
Chelsea wamewaongeza kiungo wa kati wa Leeds United na Marekani Tyler Adams, 24, na kiungo wa kati wa Ajax na Mexico Edson Alvarez, 25, kwenye orodha ya wachezaji wanaopania kuwanunua. (Times - usajili unahitajika)
&Beki wa timu ya taifa ya England chini ya miaka 21 Levi Colwill amekaribia kusaini mkataba mpya Chelsea kwa kutuma ujumbe wa kwaheri kwa Brighton kwenye mtandao wa Instagram, ambapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 alicheza kwa mkopo msimu uliopita. (TalkSPORT)
Liverpool wanatafuta mpango wa kumleta kiungo wa kati wa Fluminense wa Brazil Andre, 22, katika klabu hiyo baada ya Southampton kukataa ombi lao la pili kumnunua kiungo wao wa kati wa Ubelgiji Romeo Lavia, 19. (Sky Sports)
Beki wa Ireland Kaskazini Jonny Evans, 35, anatazamiwa kupewa kandarasi ya mwaka mmoja na Manchester United baada ya kujiunga na klabu hiyo kwa muda mfupi msimu huu. (Belfast Telegraph)
Paris St-Germain wameanzisha kipengele cha kutolewa cha euro 50m (£43m) kumsajili winga wa Barcelona na Ufaransa Ousmane Dembele, 26. (Fabrizio Romano)
West Ham wameachana na mpangowa kumnunua kiungo wa kati wa Southampton Muingereza James Ward-Prowse, wakiamini kwamba thamani ya Saints ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 iko juu sana. (Sky Sports)
Winga wa Manchester City Mreno Carlos Borges, 19, anakaribia kujiunga na Ajax kwa mkataba wa thamani ya euro milioni 20. (Athletic- Usajili unahitajika)
Everton wanaweza kumnunua mshambuliaji wa West Ham kutoka Jamaica Michail Antonio baada ya mchezaji huyo wa miaka 33 kushindwa kuhamia Saudi Arabia. (Football Insider)
Galatasaray wanamtaka kiungo wa kati wa Tottenham na Ufaransa Tanguy Ndombele na wanatumai kusaini mkataba wa pauni milioni 11 kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 (Mirror)
Leeds wanafikiria kumnunua beki wa Manchester United mwenye umri wa miaka 22 Brandon Williams. (Independent)
BBC



