Tamasha la Singida lililopewa jina la Singida Big Day limehitimisha kwa Singida FG kuibuka na ushindi wa mabao 2-1
Tamasha hilo lilikuwa maalum kwa ajili ya utambulisho wa kikosi cha Singida FG, lilifuatiwa na dakika 90 zenye ushindani kutoka kwa kila timu
AS Vita walitangulia kufunga bao kupitia kwa Ngoma Manianga kabla ya Malouf Tchakei hajairejesha mchezoni Singida FG na Dickson Ambundo kufunga bao la pili kabla ya mapumziko
Baadhi ya nyota waliopata nafasi katika mchezo huo kwa upande wa Singida FG ni Joash Onyango, Gadiel Michael na Habibu Kiyombo waliosajiliwa kutoka klabu ya Simba wakati Ambundo akitua kutoka klabu ya Yanga
Winga Mkenya Duke Abuye nae alianza katika mchezo huo
