Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, ameiambia Chelsea kwamba yuko tayari kujiunga nao kutoka Paris St Germain kwa mkataba wa mwaka mmoja akiwa ataruhusiwa kuhamia Real Madrid kwa uhamisho wa bure msimu ujao. (Sport - kwa Kihispania)
Manchester United wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo wa Southampton na Ubelgiji Romeo Lavia baada ya ombi la Liverpool kukataliwa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19. (Independent)
Uthibitisho wa United wa kumsajili mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund kutoka Atalanta unaweza kucheleweshwa hadi wikendi baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 kuwasili baadaye kuliko ilivyopangwa huko Manchester Jumanne. (Manchester Evening News)
Mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 30, yuko tayari kutoa sehemu kubwa ya mshahara wake Tottenham ili kusaidia kuhamia Bayern Munich. (Bild - kwa Kijerumani)
Spurs wanakaribia kumsajili mlinzi wa Wolfsburg Mholanzi Micky van de Ven baada ya kuafikiana na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (Talksport)
Klabu hiyo pia inatazamia kukamilisha mauzo ya kiungo wa Denmark Pierre-Emile Hojbjerg, 27, ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa pauni milioni 30 kwa Atletico Madrid. (90 min)
Inter Milan wana nia ya kumleta mlinzi wa Arsenal Mjapani Takehiro Tomiyasu, 24, katika klabu hiyo. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)
Barcelona wako kwenye mazungumzo na Manchester City kuhusu kumnunua beki wa pembeni wa Ureno, Joao Cancelo, 29. (Talksport)
Manchester United wameanza mazungumzo na Real Sociedad kuhusu mauzo ya kiungo wa Uholanzi Donny van de Beek, 26, ambayo yatasaidia kufadhili uhamisho wa kiungo wa kati wa Fiorentina mwenye umri wa miaka 26 wa Morocco, Sofyan Amrabat. (Mail)
Chelsea wanakabiliwa na ushindani katika usajili wa kiungo wa Brighton na Ecuador Moises Caicedo huku klabu ambayo bado haijatambulika ikivuka dau la pauni milioni 80 la The Blues kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. (Athletic - Usajili unahitajika)
The Blues wanatarajiwa kujibu hatua hiyo kwa ofa iliyoboreshwa ili kumnasa Caicedo, ambaye thamani yake inakaribia pauni milioni 100 kulingana na Brighton. (Sky Sports)
Aston Villa wamejiunga na kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa kati wa Leeds United Tyler Adams na wako tayari kukutana na mchezaji huyo wa kimataifa wa Marekani mwenye umri wa miaka 24 kwa pauni milioni 25. (Mail)
West Ham wanatafuta mbadala wa kiungo wa kati wa Southampton Muingereza James Ward-Prowse baada ya dau la pauni milioni 30 la kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 kukataliwa. (Sky Sports)
Al-Nassr wanamenyana na Tottenham na wanatarajiwa kulipa euro 15m (£13m) kwa ajili ya kuinasa saini ya beki wa Barcelona mwenye umri wa miaka 28, Clement Lenglet. (Sport - kwa Kihispania)
Luton wamekubali ada ya pauni milioni 2.5 pamoja na nyongeza na Blackburn kwa mlinda mlango wa Ubelgiji Thomas Kaminski, 30. (Athletic - usajili unahitajika)
nter Milan wanatazamia kuongeza dau lao la kumnunua mshambuliaji wa West Ham Gianluca Scamacca, 24, hadi pauni 21.5m huku wakijaribu kumrejesha mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia kwenye Serie A. (Evening Standard)
Willian wa Fulham amepokea ofa kutoka kwa klabu ya Saudi Arabia Al-Shabab wiki mbili na nusu pekee baada ya winga huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 34 kukubaliana kandarasi ya mwaka mmoja na klabu hiyo ya London (Athletic - usajili unahitajika)
Bournemouth wako kwenye mazungumzo ya hali ya juu na wako tayari kuipiku Wolves kwenye usajili wa kiungo wa Bristol City Mwingereza Alex Scott kwa pauni milioni 25. (Telegraph - usajili unahitajika)
Everton wanamfuatilia mshambuliaji wa Southampton na Ghana Kamaldeen Sulemana, 21, kama mbadala wa winga wa Leeds United, 19 wa Italia, Wilfried Gnonto. (Football Insider)
Besiktas wanakaribia kumsajili winga wa Arsenal wa Ivory Coast, Nicolas Pepe, 28. (Transfermarkt - kwa Kituruki)
Klabu hiyo ya Uturuki pia iko kwenye mazungumzo na kiungo wa Uingereza Alex Oxlade-Chamberlain, 29, baada ya mkataba wake na Liverpool kumalizika msimu huu wa joto. (Express)
Nottingham Forest na West Ham United ni miongoni mwa vilabu vinavyomwania mshambuliaji wa Paris-Saint Germain Mfaransa Hugo Ekitike, 21. (RMC Sport - kwa Kifaransa)
BBC



