Klabu ya Tabora united imemsajili mshambuliaji raia wa Ghana Eric Okutu(25) kutoka klabu ya Hearts of Lions FC ya ligi kuu nchini Ghana kwa mkataba wa miaka miwili
Timu hiyo pia imemsajili Kelvin Kingu Pemba beki wa kati kutoka katika klabu ya Mbabane Swallows kwa Mkataba wa miaka Miwili
Mutuale Ngonyai kiungo kutoka katika klabu ya Maniema FC ya ligi kuu Dr Congo kwa mkataba wa mwaka mmoja na Andy Bikoko Lobuka kutoka klabu ya SM Sanga Balende FC ya ligi kuu DR Congo kwa mkataba wa miaka miwili
Hivi karibuni Tabora United ilikamilisha Uhaamisho wa golikipa John Noble kutoka klabu ya Enyimba ya Nigeria, Noble alisaini mkataba wa mwaka mmoja



