Tabora United yaendelea kushusha wa Kimataifa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd August 2023


Tabora United yaendelea kushusha wa Kimataifa

Klabu ya Tabora united imemsajili mshambuliaji raia wa Ghana Eric Okutu(25) kutoka klabu ya Hearts of Lions FC ya ligi kuu nchini Ghana kwa mkataba wa miaka miwili

Timu hiyo pia imemsajili Kelvin Kingu Pemba beki wa kati kutoka katika klabu ya Mbabane Swallows kwa Mkataba wa miaka Miwili

Mutuale Ngonyai kiungo kutoka katika klabu ya Maniema FC ya ligi kuu Dr Congo kwa mkataba wa mwaka mmoja na Andy Bikoko Lobuka kutoka klabu ya SM Sanga Balende FC ya ligi kuu DR Congo kwa mkataba wa miaka miwili

Hivi karibuni Tabora United ilikamilisha Uhaamisho wa golikipa John Noble kutoka klabu ya Enyimba ya Nigeria, Noble alisaini mkataba wa mwaka mmoja


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.