Azam Fc leo inahitimisha mechi ya mwisho kujipima nguvu dhidi ya Bandari Fc ya Kenya
Mchezo huo utapigwa uwanja wa Azam Complex, saa 11 jioni
Hakutakuwa na mashabiki na pia mchezo huo hautarushwa mbashara ukiwa maalum kwa ajili ya benchi la ufundi zaidi kuangalia utayari wa kikosi chao kuelekea Ngao ya Jamii
Azam Fc itachuana na Yanga Jumatano ijayo kwenye mchezo wa kwanza wa nusu fainali Ngao ya Jamii



