Mikiki mikiki Ngao ya Jamii kuanza leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th August 2023


Mikiki mikiki Ngao ya Jamii kuanza leo

Michuano ya Ngao ya Jamii inaanza leo jijini Tanga ambapo mchezo wa kwanza wa nusu fainali ni kati ya mabingwa watetezi Yanga dhidi ya Azam Fc

Mchezo huo utapigwa saa 1 usiku katika uwanja wa Mkwakwani

Kwa mara ya kwanza mwaka huu, Ngao ya Jamii inashirikisha timu badala ya timu mbili kama ilivyokuwa imezoeleka huko nyuma

Mchezo wa pili wa nusu fainali kati ya Simba dhidi ya Singida FG unatarajiwa kupigwa kesho Alhamisi katika uwanja wa Mkwakwani

Mshindi wa mchezo wa leo atakutana na mshindi wa mchezo kesho kwenye fainali wakati timu zitakazopoteza zitachuana kusaka mshindi wa tatu

Michezo ya fainali na mshindi wa tatu itapigwa Jumapili, August 13


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.