Simba - Local

Simba yatamba kufuata Ngao ya Jamii Tanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Aug 2023
Simba yatamba kufuata Ngao ya Jamii Tanga

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally, amesema mkakati wa Simba ni kuibuka mabingwa wa Ngao ya Jamii

Simba ilitua Tanga jana majira ya usiku na leo inatarajiwa kukamilisha maandalizi kabla ya mchezo wa nusu fainali dhidi ya Singida Fountain Gate. Mchezo huo utapigwa kesho Alhamisi katika uwanja wa Mkwakwani

"Tunashukuru tumefika salama mkoani Tanga. Leo tutakuwa na nafasi ya kufanya mazoezi ya mwisho majira ya saa 11 jioni"

"Sisi hatukuja hapa Tanga kutembelea, tumekuja kuchukua Ngao ya Jamii. Tumejiandaa vizuri na pia tuna kikosi bora, hivyo hakuna mjadala kuhusu hilo, kauli mbiu yetu ni kuwa TUMEKUJA TANGA KUCHUKUA NGAO YA JAMII," alisema Ahmed

Katika hatua nyingine, Ahmed amesema mshambuliaji Moses Phiri ni miongoni mwa wachezaji waliosafiri na timu mkoani Tanga

Ahmed amesema Phiri yuko fit kwa asilimia 100 na uongozi unamtekelezea mahitaji yake yote

"Phiri ni miongoni mwa wachezaji waliosafiri na timu mkoani Tanga, suala la kucheza au la linabaki mikononi mwa benchi la ufundi. Lakini sisi upande wa uongozi tumetimiza kile ambacho tunapaswa kufanya kwa mchezaji"

"Wanasimba wapuuze taarifa za upotoshaji kwani hakuna kiongozi anayeweza kumzuia Phiri asicheze. Haiwezekani klabu imlipe fedha nyingi halafu tumzuie asicheze, hilo haliingii akilini"

"Ni kweli Wanasimba wanataka kumuona Phiri uwanjani, hata sisi viongozi tunatamani kumuona Phiri uwanjani kwani ni mchezaji bora lakini bado mwenye maamuzi ya mwisho ni kocha Robertinho," alisema Ahmed

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’