Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi August 10 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th August 2023


Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi August 10 2023

Manchester United wanatumai kumuunganisha tena Benjamin Pavard, 27, na mchezaji mwenza wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa, beki wa kati wa Mashetani Wekundu Raphael Varane, 30, kwa kutoa ofa ya euro 30m (£25.8m) kwa mlinzi huyo wa Bayern Munich. (L'Equipe)

Manchester United pia wana nia ya kumleta Sofyan Amrabat wa Fiorentina, huku raia huyo wa Morocco mwenye umri wa miaka 26 akipatikana kwa £30m. (Mail)

Hata hivyo, Amrabat anataka kujiunga na Atletico Madrid ya Diego Simeone msimu huu wa joto. (Sport)

Maafisa wa Paris St-Germain na mshambuliaji wa Brazil Neymar watakutana wiki hii katika jaribio la kutatua mustakabali wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, na kusitishwa kwa mkataba wake ni miongoni mwa masuala yatakayojadiliwa. (UOL Sport Brasil)

Chelsea wanakaribia kumsajili kiungo wa Ecuador Moises Caicedo, 21, kutoka Brighton na wana nia ya kukamilisha usajili kwa wakati ili acheze mchezo wa ufunguzi wa ligi dhidi ya Liverpool siku ya Jumapili. (Guardian)

Kipa wa Chelsea Mhispania Kepa Arrizabalaga, 28, anasakwa na meneja wa zamani wa The Blues Thomas Tuchel aliyeko Bayern Munich huku timu hiyo ya Bundesliga ikitafuta mbadala wa Mjerumani Manuel Neuer mwenye umri wa miaka 37 ambaye ameumia. (Fabrizio Romano)

Chelsea wameamua kuachana na mazungumzo na Juventus kuhusu mkataba wa kubadilishana unaomhusisha mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 23, na mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 30. (Sky Sport Italia Via Football Italia)

Kipa wa Brentford na Hispania David Raya, 27, anatazamiwa kujiunga na Arsenal kwa mkopo akiwa na chaguo la kujiunga moja kwa moja msimu ujao, badala ya uhamisho wa kudumu. (Agthletic)

Arsenal wamekataa dau la pauni milioni 30 kutoka kwa Monaco inayoshiriki Ligue 1 kwa ajili ya mshambuliaji wao Mmarekani Folarin Balogun, 22. (90MIN)

Badala yake, Arsenal wanafikiria kuwatoa Balogun na mlinzi wa pembeni Mjapan Takehiro Tomiyasu, 24, kwenda Inter Milan ili kubadilishana na kiungo wao wa kati wa Italia Nicolo Barella, 26. (Calciomercato)

West Ham inashindana na Burnley kwa ajili ya kumnasa kwa mkopo mlinzi wa kushoto wa Chelsea Ian Maatsen, 21, ambaye alicheza kwa mkopo msimu uliopita akiwa na kikosi cha Vincent Kompany waliposhinda taji la Ubingwa. (Mail)

Burnley pia wanataka kumsajili beki wa pembeni wa Manchester United Mhispania Alvaro Fernandez kwa mkopo baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 kuonyesha kiwango kizuri akiwa Preston msimu uliopita. (Sky Sports via Twitter)

Wolves wanatarajiwa kukamilisha usajili wa beki wa West Ham Muingereza Aaron Cresswell, 33, kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Football Insider)

Mshambulizi wa Brighton raia wa Paraguay mwenye umri wa miaka 19, Julio Enciso anasakwa na mabingwa wa Italia Napoli. (Telegraph)

Bournemouth wako tayari kuingilia kati uhamisho wa Leeds United kwa beki wa kulia wa Norwich City Muingereza Max Aarons, 23. (Athletic)

Winga wa Leeds Wilfried Gnonto aliomba kuachwa nje ya kikosi chao kilichomenyana na Shrewsbury Town katika Kombe la Carabao Jumatano usiku huku Muitaliano huyo, 19, akitarajia kuhama. (Mail)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.