Klabu za Simba na Singida FG zimewasilisha vibali vya nyota wake wa kigeni kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF, Simba imewasilisha vibali vya wachezaji 11 wakati Singida FG imewasilisha vibali vya wachezaji 10
TFF iliweka zuio kwa wachezaji wa kigeni ambao hawana vibali kutoshiriki michuano ya Ngao ya Jamii
Simba na Singida FG zitachuana leo katika mchezo wa pili wa nusu fainali ambao utapigwa saa 1 katika uwanja wa Mkwakwani
Mshindi wa mchezo huo atachuana na Yanga kwenye fainali wakati timu itakayofungwa itachuana na Azam Fc katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu siku ya Jumapili




