Simba, Singida FG zawasilisha vibali nyota wa kigeni

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th August 2023


Simba, Singida FG zawasilisha vibali nyota wa kigeni

Klabu za Simba na Singida FG zimewasilisha vibali vya nyota wake wa kigeni kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF, Simba imewasilisha vibali vya wachezaji 11 wakati Singida FG imewasilisha vibali vya wachezaji 10

TFF iliweka zuio kwa wachezaji wa kigeni ambao hawana vibali kutoshiriki michuano ya Ngao ya Jamii

Simba na Singida FG zitachuana leo katika mchezo wa pili wa nusu fainali ambao utapigwa saa 1 katika uwanja wa Mkwakwani

Mshindi wa mchezo huo atachuana na Yanga kwenye fainali wakati timu itakayofungwa itachuana na Azam Fc katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu siku ya Jumapili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.