Yanga - Local

Derby sio vita, ni furaha - Gamondi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Aug 2023
Derby sio vita, ni furaha - Gamondi

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema hana wasiwasi wowote kuelekea mchezo wa fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Simba ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Mkwakwani

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Gamondi amesema ameshiriki mechi nyingi za dabi hivyo mchezo huo hautakuwa tofauti

Aidha, kocha huyo raia wa Argentina amesema mchezo huo hautakuwa vita, anaamini ni mechi nzuri ya kuwapa furaha mashabiki

"Ni Furaha kwangu kucheza dabi kesho na haitakuwa na presha kwani nimeshakutana na dabi nyingi hapo kabla. Hii siyo vita ni mpira wa miguu, ukishinda au kufungwa maisha yanaendelea"

"Huu ni mchezo ambao majukumu yangu kama kocha sio makubwa sana, wachezaji wanafahamu wanacheza kwa ajili ya mashabiki wao ambao watajitokeza kwa wingi kuwashangalia. Nimesimamia dabi nyingi nikiwa Sundowns, Wydad, Raja, Etoile Sahel na nyingine"

"Ninatamani nicheze hata mechi 30 za msimu mzima dhidi ya Simba kwa sababu ni dabi ambayo wachezaji wako tayari wakati wowote kuicheza," alisema Gamondi

Mlinzi wa kati Dickson Job amesema maandalizi yamekamilika na wanasubiri siku ya kesho ifike ili waweze kushuka dimbani kuwapa furaha mashabiki wao

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’