Simba - Local

Robertinho afurahia taji la kwanza la msimu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Aug 2023
Robertinho afurahia taji la kwanza la msimu

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amewapongeza wachezaji, viongozi wa Simba na mashabiki kwa umoja na ushirikiano ambao umepelekea wakashinda taji la kwanza msimu huu

Simba imetwaa Ngao ya Jamii baada ya ushindi wa mikwaju ya penati 3-1 dhidi ya Yanga katika mchezo wa fainali uliopigwa jana katika uwanja wa Mkwakwani

Dakika 90 za mchezo huo zilimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana, hivyo mshindi kuamuliwa kwa changamoto ya penalti

Mlinda lango wa Simba Ali Salim alikuwa shujaa katika mchezo huo akiokoa penalti tatu

"Nafurahi tumetimiza malengo yetu. Tulitarajia mchezo utakuwa mgumu kwa sababu hakuna mechi ya derby rahisi, lakini sisi tuliingia na mkakati wetu ambao wachezaji waliukamilisha"

"Nafikiri tulicheza vizuri kwenye kipindi cha kwanza tukiwa na mpira na hata bila ya mpira. Kipindi cha pili tulifanya mabadiliko ya uchezaji na baadhi ya wachezaji ili kuongeza presha katika lango la wapinzani"

"Nawapongeza wachezaji wangu, nampongeza kipa wetu (Ally Salim) ni kijana mdogo lakini tangu msimu uliopita kwenye ligi ya mabingwa amekuwa mchezaji muhimu kwetu"

"Nampongeza kila mmoja, sote tumeshirikiana kupata mafanikio haya, tumeshinda taji la kwanza msimu huu," alisema Robertinho

Salim anastahili tuzo ya nyota wa mchezo huo jana lakini pia pengine ndiye mchezaji bora wa michuano ya Ngao ya Jamii kwani hata katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya Singida FG, alidaka mkwaju wa penati na kuisaidia Simba kutinga fainali

Kwa hakika Salim ameonyesha ukomavu na pengine ataleta ushinda katika eneo la golikipa ambalo juzi Simba ilimuongeza Ayoub Lakred kutoka Morocco

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
21h ago
READ MORE β†’