Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo kwa mchezo mmoja kupigwa mkoani Morogoro
Mtibwa Sugar watawakaribishwa mabingwa wapya wa Ngao ya Jamii, Simba Sc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Manungu, Turiani
Huu ni mchezo wa kwanza kwa kila timu msimu huu, Simba ikiwa na hesabu za kutwaa ubingwa wakati Mtibwa Sugar wamepania kutorudia makosa ya misimu iliyopita ambayo yalipelekea timu hiyo kuponea kushuka daraja katika mechi za play-off
Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kwa ubora wa kikosi chake ana kila sababu ya kushinda mchezo huo wakati Afisa Habari wa Mtibwa Thobias Kifaru akibainisha kuwa wanawaheshimu Simba lakini wasitarajie mchezo mwepesi kutoka kwao
Mara ya mwisho timu hizo ziilipokutana msimu uliopita katika uwanja wa Manungu, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 mshambuliaji Jean Baleke akifunga mabao yote
Baleke amerejea tena Manungu kuwawinda tena Mtibwa Sugar