Baada ya kupoteza mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Geita Gold, jana Ihefu ilimalizia machungu yake kwa Kagera Sugar baada ya kuwalaza bao 1-0 mchezo uliochezwa Uwanja wa Highland Estate jijini Mbeya
Bao la Mubaack Amza mshambuliaji wa zamani wa Coastal Union, liliihakikishia Ihefu Fc ushindi huo muhimu katika uwanja wa nyumbani
Kwa upande wa Kagera Sugar wameanza vibaya msimu wakipoteza mechi zote mbili za ufunguzi
Kabla ya kipigo cha jana, Kagera Sugar walianza kwa kuchapwa mabao 2-0 na Mashujaa Fc katika mchezo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma
Kocha Mkuu wa Kagera Sugar Meckie Mexime amelia na ratiba akibainisha kuwa timu yake ilikosa muda wa kupumzika wakiwasili Mbeya majira ya saa 5 usiku wa kuamkia mchezo huo
Nao KMC wamefanikiwa kuondoka na alama moja Ruangwa baada ya sare ya bao 1-1 dhidi y wenyeji wao Namungo Fc