Simba yapanda kileleni Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th August 2023


Simba yapanda kileleni Ligi Kuu

Mnyama ameunguruma uwanja wa Uhuru akiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Jean Baleke ameendeleza kasi yake ya kupachika mabao msimu huu, leo akifunga bao lake la pili katika mchezo wa pili mfululizo

Bila shaka kocha wa Simba Robertinho Oliveira leo ameelewa kwa nini Wanasimba wanashinikiza Jenerali Moses Phiri kupewa nafasi ya kucheza leo akifunga bao la pili kwa Simba

Ni ushindi ambao umeipeleka Simba kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama sita

Mwendo wa kukusanya alama tatu kila mchezo mpaka ubingwa...!

Katika mchezo uliopigwa mapema, Mtibwa Sugar imelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Coastal Union katika mchezo uliopigwa uwanja wa Manungu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.