Mnyama ameunguruma uwanja wa Uhuru akiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo wa ligi kuu ya NBC
Jean Baleke ameendeleza kasi yake ya kupachika mabao msimu huu, leo akifunga bao lake la pili katika mchezo wa pili mfululizo
Bila shaka kocha wa Simba Robertinho Oliveira leo ameelewa kwa nini Wanasimba wanashinikiza Jenerali Moses Phiri kupewa nafasi ya kucheza leo akifunga bao la pili kwa Simba
Ni ushindi ambao umeipeleka Simba kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama sita
Mwendo wa kukusanya alama tatu kila mchezo mpaka ubingwa...!
Katika mchezo uliopigwa mapema, Mtibwa Sugar imelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Coastal Union katika mchezo uliopigwa uwanja wa Manungu



