Kiungo Baraka Majogoro anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya Chippa United ya Afrika Kusini, amesema licha ya kutopata nafasi ya kuanza kikosi cha kwanza anaamini muda utafika
Majogoro alijiunga na Chippa inayoshiriki Ligi Kuu nchini Afika Kusini na amekaa benchi kwenye mechi mbili kati ya tatu za mwanzo hadi ya juzi (Jumamosi) dhidi ya Mamelod ndio ulikuwa mchezo wa nne na walifungwa mabao 2-0
Majogoro amesema kitendo cha yeye kuwa kati ya wachezaji 20 katika mchezo husika, kwake ni jambo kubwa licha ya kutopata nafasi ya kucheza
"Nafasi ipo ila inahitaji upambanaji kwa sababu hapa nimekuta watu waliokuwepo, naheshimu uwezo wao lakini nitakapopata nafasi nitapambana. Kweli nimekaa benchi mechi mbili na tumecheza mechi na Mamelod na nipo kwenye kikosi cha watu 20 kambini kwahiyo inaonyesha natakiwa kuwa tayari, nafasi ni suala la muda," alisema
Majogoro alisajiliwa na Chippa United akitokea klabu ya Mtibwa Sugar aliyoitumikia kwa msimu mmoja
Alipata nafasi ya kusajiliwa baada ya kufuzu majaribio



