Mabingwa watetezi ligi kuu ya NBC Yanga wameanza msimu kibabe baada ya kuibamiza KMC mabao 5-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi Yanga ikitawala zaidi
Ilikuwa ni suala la Yanga kufunga mabao mangapi katika mchezo huo
Nahodha wa Yanga katika mchezo huo Dickson Job alifungua akaunti ya mabao kwa upande wa Yanga kwa kufunga bao la kwanza mapema kwenye kupindi cha kwanza
Mambo yalizidi kuwa magumu zaidi kwa KMC kwenye kipindi cha poili ambapo waliruhusu mabao mengine manne yaliyofungwa na Stephane Aziz Ki, Hafiz Konkoni, Mudathir Yahya na Pacome Zouzoua
Ni ushindi ambao umeipandisha Yanga mpaka nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi, alama tatu kutoka mechi moja na mabao matano ya kufunga

