Yanga yatangaza viingilio mchezo dhidi ya Asas Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th August 2023


Yanga yatangaza viingilio mchezo dhidi ya Asas Fc

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amewataka Wanachama na Mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Azam Complex siku ya Jumamosi, August 26 katika mchezo wa mkondo wa pili ligi ya mabingwa barani Afrika hatua ya awali dhidi ya Asas Fc

Kamwe amesema wanahitaji kushinda mchezo huo ili kujihakikishia tiketi ya kutinga raundi ya kwanza ya michuano hiyo ikiwa ni hatua moja kuelekea makundi

"Mchezo huu haujamalizika kama wengi wanavyosema. Unapodharau mpinzani kwa sekunde moja tu, mechi inaweza kubadilika. Iko mifano mingi tu, kuna timu ziliwahi kushinda ugenini na kupoteza nyumbani"

"Kwa kuwa tuna dakika 90 za kucheza hatupaswi kuwadharau wapinzani wetu. Tunaomba mashabiki wetu mje kwa wingi kushangilia ili kuhakikisha tunasonga mbele. Nawaomba mashabiki tusiingie katika mtego wa kudhani mechi imemalizika"

Kamwe ametangaza viingilio vya mchezo huo ambapo Mzunguuko ni Tsh 5,000/-, VIP B ni Tsh 20,000/- na VIP A ni Tsh 30,000/-

Kamwe amewaasa mashabiki kuhakikisha wananunua tiketi zao mapema, wasisubiri kukata tiketi uwanjani kwani kuna matukio ya kuuziwa tiketi feki

Aidha Kamwe amesema siku hiyo imepewa jina la 'Max Day', Wananchi wataitumia kumuenzi mchezaji wao Max Nzengeli kwa kuchomekea

"Kwa yeyote atakayekuja uwanjani ahakikishe amechomekea, huu ndio utakuwa mtoko wetu wa Max Day," alisema Kamwe


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.