Kiungo wa kati wa Crystal Palace na Mali Cheick Doucoure, 23, yuko juu ya orodha ya Liverpool inayowania kiungo mpya na thamani yake ni £70m. (Football Insider)
Manchester United wamewasiliana na Chelsea kuhusu kumnunua kwa mkopo mchezaji wa Uhispania Marc Cucurella, 26. (Fabrizio Romano)
Mshambuliaji wa Liverpool na Misri Mohamed Salah, 31, ameiambia klabu hiyo anataka kujiunga na klabu ya Saudi Arabia ya Al-Ittihad. (Rudy Galetti)
Mlinzi wa Arsenal na Scotland Kieran Tierney, 26, ametua Uhispania kukamilisha uhamisho wa kwenda mkopo Real Sociedad. (Fabrizio Romano)
Kiungo wa kati wa Uingereza Connor Gallagher, 23, atakataa kuhamia Tottenham ili kupigania nafasi yake Chelsea. (Football Insider)
Ajax wako kwenye mazungumzo na Atlanta United kuhusu dili la kiungo wa Argentina Thiago Almada, 22. (90 min)
Chelsea wanalenga kumnunua mlinzi wa Bayer Leverkusen na Uholanzi Jeremie Frimpong, 22. (Fichajes - kwa Kihispania)
Brighton wamekubali mkataba wa pauni milioni 23.2 kumsaini kiungo wa kati wa Lille na Cameroon Carlos Baleba, 19. (Sport)
Mlinzi wa pembeni Ivan Fresneda, 18, anatarajiwa kujiunga na Sporting Lisbon kutoka Real Valladolid. Alihusishwa na Arsenal na Newcastle. (Fabrizio Romano)
Barcelona pia walikuwa wakimtaka Fresneda lakini wakachagua kumsajili Joao Cancelo, 29, kutoka Manchester City. (Athletic)
Crystal Palace inaweza kumpa kiungo wa kati wa Uingereza Eberechi Eze, 25, kandarasi ya pauni milioni 5 kwa mwaka na kifungu cha kutolewa huku kukiwa na nia ya Manchester City. (Sun)
Sevilla wameuliza kuhusu uwezekano wa kumsajili tena mlinzi wa Ufaransa Clement Lenglet, 28, kutoka Barcelona. (Marca in Spanish)
Mkufunzi wa Fiorentina Vincenzo Italiano anaitaka bodi kutafuta suluhu la kiungo wa kati wa Morocco Sofyan Amrabat mwenye umri wa miaka 27 licha ya Manchester United kumtaka. (Sky Germany)
BBC



