Kiungo mshambuliaji Peter Banda anaondoka klabu ya Simba kusaka changamoto mahali pengine baada ya makubaliano ya pande mbili
Banda alikuwa bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Simba lakini makubaliano yamefikiwa, Simba ikimruhusu aondoke
Banda huenda akajiunga na Fc Kyrvbas inayoshiriki Ligi Kuu ya Ukraine
Ameitumikia Simba kwa misimu miwili hata hivyo Wanasimba hawakufaidi kipaji chake kutokana na majeraha yaliyokuwa yakimkabili mara kwa mara



