Yanga - Local

Yanga kumlipa Bigirimana kwa awamu

Joel JJ By Joel JJ
31 Aug 2023
Yanga kumlipa Bigirimana kwa awamu

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema Yanga itamlipa kwa awamu aliyekuwa kiungo wake Gael Bigirimana

Kulikuwa na mvutano kati ya uongozi wa Yanga na mchezaji huyo juu ya malipo aliyokuwa akihitaji ili kuvunja mkataba wake wa mwaka mmoja uliokuwa umebaki hivyo kupelekea pande hizo kupelekana FIFA kwa ajili ya kupata suluhisho

FIFA ikatoa maamuzi  ya kuitaka Yanga imlipe Bigirimana kiasi cha fedha walichokuwa wamekubaliana na kwa kuwa Yanga ilichelewa kukamilisha malipo ya awamu ya kwanza ambayo walipaswa kulipa ndani ya siku 45 tangu hukumu ilipotolewa, juzi TFF wakatoa taarifa kuwa Yanga imefungiwa na FIFA kusajili hadi hapo watakapomlipa mchezaji huyo

Kamwe amethibitisha kuwa mchakato wa malipo ya Bigirimana unaendelea huku akiwatoa hofu Wanachama na Mashabiki wa Yanga kuwa jambo hilo litamalizwa hivi karibuni

Dirisha la usajili linafungwa leo, ahueni kwa Yanga ni kuwa hukumu hiyo imetolewa wakati wakiwa tayari wamekamilisha michakato ya usajili katika dirisha hili  

Ili Yanga iweze kusajili wachezaji katika madirisha yajayo ni lazima ikamilishe malipo ya Bigirimana ambaye usajili wake ni kama umesababisha hasara tu kwani hakufikia hata nusu ya kile ambacho wengi walitarajia kutoka kwake hasa ikizingatiwa ni mchezaji aliyewahi kucheza ligi kuu ya Uingereza

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
51m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
1h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
2h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
2h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
2h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
2h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
3h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
14h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
15h ago
READ MORE →