Kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Novatus Dismas Miroshi mwenye umri wa miaka 21 amejiunga na klabu ya Shakhtar Donesk ya Ukraine akitokea klabu ya Zulte Waregem ya Ubelgiji
Novatus atacheza UEFA Champions League akiwa na Shakhtar
Mabingwa hao wa Ukraine wapo kundi H pamoja na timu za Barcelona, Porto na Royal Antwer
Atakuwa Mtanzania wa pili kucheza michuano hiyo mikubwa zaidi kwa ngazi klabu barani Ulaya baada ya Mbwana Samatta aliyewahi kushiriki michuano hiyo akiwa na KRC Genk



